Wednesday, September 11, 2013

HODGSON APUMUA INGAWA KAZI IPO, ATOKA 0-0 NA UKRAINE, MECHI DHIDI YA MONTENEGRO NA POLAND NDIO MAHAKAMA YAKE!!

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
MENEJA wa Timu ya Taifa ya England, maarufu `Simba Watatu`, Roy Hodgson amepumua kidogo katika harakati zake za kuwania kucheza fainali za kombe la Dunia mwakani nchini Brazi baada ya kutoka suluhu dhidi ya Ukraine jana usiku.
England iliingia uwanjani kupambana kwa nguvu bila ya nyota wake Wayne Mark Rooney, Dany Welbeck na Daniel Sturrage kutokana na sababu tofauti.
Sturrage na Rooney ni majeruhi, wakati Welbeck alikuwa anatumikia kadi aliyopewa mechi ya nyuma.
Juni 19, 2012, ilikuwa mara ya mwisho kwa England kushinda mechi ya ushindani, lakini si dhidi ya Moldova au San Marino bali Upinzani wa siku hiyo ulikuwa dhidi ya Ukraine, na toka hapo, England imeshakutana mara mbili na wakali hao na kushindwa kuibuka na ushindi.
England wamebakiwa na mechi dhidi ya Montenegro pamoja na Poland mwezi ujao na wanatakiwa kupata ushindi ili kukata tiketi ya  kcuheza fainali za kombe la Dunia mwakani nchini Brazil.
Na mechi hizo watacheza katika dimba lao la Taifa la Wembley, hivyo kujipa matumaini ya kufanya vizuri.
Late drama: Frank Lampard heads one just past the post in second half stoppage timeDuuh!: Frank Lampard akipiga kichwa na kugonga mwamba dakika za majeruhi kipindi cha pili
Right place right time: Steven Gerrard nips in to stop Yarmolenko as Joe Hart gets ready to make a saveSehemu  na muda sahihi: Steven Gerrard akimdhibiti Yarmolenko huku Joe Hart akiwa tayari kuokoa
Centurion: Frank Lampard (left) gets a header on goal during his 100th capKapiga mechi ya 100: Frank Lampard (kushoto)  akipiga kichwa golini katika mechi yake ya 100
Deep in thought: Roy Hodgson looks to have a lot on his mind on the touchlineDimbwi la mawazo: Roy Hodgson akionekana kutoamini kinachoendeleaDesperate dive: Joe Hart flings himself across goal as Yevhen Konoplyanka's free kick is deflected wideKazi ya nguvu: Joe Hart akijaribu kuokoa mpira wa adhabu uliochongwa na Yevhen Konoplyanka
Kikosi cha Ukraine: Pyatov, Fedetskiy, Khacheridi, Kucher, Shevchuk, Stepanenko, Edmar, Gusev (Bezus 68), Yarmolenko (Khomchenovskiy 90), Konoplianka, Zozulya (Seleznyov 90). Subs: Koval, Dedechko, Tymoschuk, Mandzyuk, Grechyshkin, Morozyuk, Rakitskiy, Devic,
Khudzamov.
Kikosi cha England: Hart, Walker, Cahill, Jagielka, Cole, Lampard, Gerrard, Wilshere (Young 68), Walcott (Cleverley 89), Lambert, Milner. Subs: Ruddy, Smalling, Baines, Caulker, Carrick, Barkley, Defoe, Sterling, Townsend, Forster.

0 comments: