This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, April 13, 2013

Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo…
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
ametoa taarifa yake ya mwaka 2011/2012 na kuonyesha kuwa kuna skandali kubwa
sana katika akaunti ya Deni la Taifa. Nanukuu

‘Uhakiki wa mchanganuo wa madeni ya Taifa kama ulivyokuwa tarehe 30
Juni, 2012 ulibaini kuwepo kwa marekebisho ya deni ya shilingi
619,803,554,183.91 ambayo uongozi haukuweza kutoa maelezo ya kuridhisha.’
(Taarifa ya CAG, Ripoti ya Serikali Kuu 2011/2012 uk 158).
Mwisho wa Kunukuu



Katika Taarifa yake hiyo CAG anaendelea kuonyesha
kuwa Deni la Taifa linazidi kukua na mwaka unaoishia mwezi Juni 2012 deni
lilikuwa kwa asilimia 17 kutoka mwaka unaoishia mwezi Juni 2011.

Kukosekana kwa maelezo ya kuridhisha kuhusu zaidi
ya nusu trilioni za Deni la Taifa ni jambo linalopaswa kutiliwa mashaka
makubwa, kuchunguzwa na kupata majawabu stahiki. Tafiti mbalimbali duniani
zinaonyesha kuwa kuna mahusiano makubwa sana kati ya Deni la Taifa la
utoroshaji wa fedha kwenda kwenye mabenki ya ‘offshore’. Katika kitabu cha
‘Africa’s Odious Debts: How Foreign Loans and Capital flight bled a continent’
kilichoandikwa mabwana Leonce Ndikumana na James Boyce imeonekana kwamba Deni
la Taifa huchochea utoroshwaji wa Fedha kwenda kuficha nje ya Tanzania.

Mabilioni haya kwenye akaunti ya Deni la Taifa
yanashtusha sana. Kambi ya Upinzani Bungeni kwa miaka miwili mfululizo imekuwa
ikitaka ukaguzi maalumu kwenye akaunti za Deni la Taifa lakini Serikali
imeshindwa kufanya hivyo. Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC pia nimemtaka CAG
afanye ukaguzi huu maalumu.

Kambi ya upinzani Bungeni ilisema hivi katika
Bajeti yake kivuli 2012/13:

DENI LA TAIFA

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inasikitika kwa serikali kuendelea kutengeneza
madeni kwa Taifa kwa kuendelea kukopa zaidi kwa matumizi ya kawaida ya
serikali. Wakati Serikali inasisitiza kwamba Deni letu linastahmilika, Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Serikali anaonyesha mashaka makubwa sana kutokana na kasi ya
kukua kwa Deni la Taifa. Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali inaonyesha  kuwa Deni la Taifa
linazidi kuongezeka kwa asilimia 38% kutoka shilingi trillion 10.5 mwaka
2009/2010 hadi shilingi trillion 14.4 mwaka 2010/2011. Kwa mujibu wa Waziri wa
Fedha Deni la Taifa limefikia shilingi trillion 20.3 mpaka ilipofika mwezi
Machi mwaka 2012. Ukisoma taarifa ya Mwezi wa Mei 2012 ya Benki Kuu ya
Tanzania, Deni la Taifa sasa limefikia shilingi trillion 22.



Mheshimiwa Spika, Suala hapa sio ustahmilivu wa
Deni kama inavyodai Serikali bali ni kwamba tunakopa kufanyia nini? Bajeti ya
Mwaka 2012/13 inayopendekezwa inaonyesha kwamba Serikali itakusanya shilingi
trilioni 8.7 kama makusanyo ya ndani na itatumia shilingi trilioni 10.6 kama
matumizi ya kawaida. Ni dhahiri kwamba sehemu ya mikopo ambayo serikali
inachukua sasa itakwenda kwenye matumizi ya kawaida. Hatutaki mikopo kwa ajili
ya matumizi ya kawaida ya posho, kusafiri, magari nk. Tuchukue mikopo kuwekeza
kwenye miradi itakayokuza uchumi na kuzalisha kodi zaidi. Bajeti inaonyesha kwamba
Serikali itakopa shilingi takribani trillion 5 mwaka 2012/13.  Serikali ikubalikutekeleza mapendekezoya
Kambi ya Upinzani ya kuimarisha ukusanyaji
wa kodi na kupanua wigo wa kodi katika maeneo muhimu kama sekta ya
madini na mawasiliano, kuzuia misamaha ya kodi, kutokomeza ukwepaji kodi, na
kuepuka matumizi mabaya ili kuepuka madeni yasiyo ya lazima.

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inapenda
kusisitiza kwamba Bunge lifanye ukaguzi maalumu kuhusu akaunti ya Deni la Taifa
ili kuweza kubaini ukweli kuhusu ustahmilivu wa Deni na mikopo ambayo Serikali
inachukua kama inakwenda kwenye Maendeleo na miradi ipi na kama miradi hiyo ina
tija. Vilevile tumependekeza kwamba Mikopo yote ambayo Serikali inachukua iwe
inapata idhini ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi au Bunge litunge sharia
ili kiwango cha juu cha kukopa ambacho Serikali haipaswi kuvuka. Kuiacha
Serikali inaendelea kukopa bila mpango ni kuliweka Taifa rehani na kupeleka
mzigo wa kulipa madeni haya kwa kizazi kijacho. Hatuwezi kukubali Wazee wetu waishi maisha yao, waishi maisha yetu na
pia wakope maisha ya watoto wetu.
Mwisho wa
kunukuu.

Kambi ya Upinzani inarejea kutaka
ukaguzi maalumu kuhusu akaunti za Deni la Taifa na maelezo ya kina ya Serikali
kuhusu shilingi 620 bilioni ambazo hazina maelezo kwenye Deni la Taifa.
Hatuwezi kukaa kimya kuona Watanzania wanabebeshwa madeni ambayo kimsingi ni
madeni bandia yanayotajirisha watu wachache wenye uwezo na ujasiri mkubwa wa
kuiba, kupora nakufisidi hazina ya Taifa letu.

Friday, April 12, 2013

MAKALI YA NAULI KUANZA KUFANYAKAZI

DSCF9477 86da1
Hizi nauli zilivyopanda kwa mamlaka ya wenyemaamuzi hivi hawa Nduguzangu wa ishio mwambao wa ziwa Nyasa itakuwaje?
Waungwana naomba mawazoyenu pamojanakuwa halihiyo inatukumba sote lakini kwa hali yakimaisha tunatofautiana kwa tulio mijini na vijijini.

Tena tunavyo tafuta kipato kwakutumia fursa tulizonazo katika maeneo tofauti naimani wenzetu waishio
Mwambao wa Ziwa Nyasa wilaya ya Ludewa itawawea vigumu mmno kwasababu hali yauchumi kwao ningumu . kwani wanategemea uvuvi na baada ya kuvua wanategemea usafiri wa Boti kwenda Matema Kyela mkoa wa Mbeya kuuza nakujipatia mahitaji muhimu. Usafili huo hupatikana kwa wiki malamoja.
Kwani wananchi hao hawana usafili waaina nyingine wowote hakuna Barabala wala njia yakupitisha pikipiki au Baiskeli.
Mwishoni mwa mwaka 2012, nikiwa katika ziara ya mbunge nilishuhudia wananchi wakimshukuru mbunge wao Deo Filikunjombe alipowatembelea nakuwaeleza matarajio ya maendeleo aliyo waahidi wakati wa uchaguzi
Kamavile kuwaboreshea usafiri wa Meli,Boti,na njia za mawasiliano yasimu kwamshangao walionyesha furaha iliowatoa machozi kwakuwa kwao nindoto kusikia maelezohayo. Sasa wakatihayo yakifanyiwa mchakato kwa utekelezaji Mzigo mwingine unakuja ambao haukwepeki.
Niwazi wenye vyombo vya usafilishaji majini hawatakwepa kuongeza bei.
Nduguzangu nakumbuka unapoumwa binafsi huhisi hakuna anae umwa zaidi yako lakini ufikapo Hospitali utawakuta wanaoumwa zaidi yako na utawapisha wamuone Mganga ndivyo ilivyo kwa wenzetu waishio Mwambao wa ziwa nyasa hakuna l msaada wadharula kwa wazima au wagonjwa.
MWISHO.

MAMA SHARO AANZA KUKOMALIA HAKI ZA MWANAYE

Na Gladness Mallya

MAMA mzazi wa aliyekuwa msanii wa muziki na filamu Bongo, marehemu Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’, Bi. Zainabu Mkieti amefunguka kuwa kwa sasa anaanza kufuatilia haki za mwanaye kwenye kampuni alizokuwa anafanya nazo kazi kwani tayari ameshafungua mirathi.
Marehemu Hussein Ramadhan Mkieti 'Sharo Milionea'.
Akichezesha taya na paparazi wetu kwa njia ya simu akiwa jijini Tanga, Mama Sharo alisema tayari ameshafungua mirathi na msimamizi ni mama mkubwa wa Sharo anayejulikana kwa…

REEBOK WAMTOSA RICK ROSS KUTOKANA NA MASHAIRI YAKE YANAYOSIFIA UBAKAJI



Baada ya wiki kadhaa za ukosoaji na maandamano, kampuni ya Reebok imesitisha kufanya kazi na Rick Ross kutokana na mashairi yake yenye kashfa ya kusifia vitendo vya ubakaji.
Wimbo wa Rick Ross unaodaiwa kuwa na mashairi ya kupromote ubakaji unaitwa “U.O.E.N.O.”

Katika maelezo iliyoutumia mtandao wa TMZ, Reebok imesema:

“Reebok holds our partners to a high standard, and we expect them to live up to the values of our brand. Unfortunately, Rick Ross has failed to do so.

While we do not believe that Rick Ross condones sexual assault, we are very disappointed he has yet to display an understanding of the seriousness of this issue or an appropriate level of remorse.”
Rick-Ross-Gets-Dumped-By-Reebok-4

Kwenye “U.O.E.N.O,” Ross anarap: “Put molly all in her champagne, she ain’t even know it. I took her home and I enjoyed that, she ain’t even know it.”

Mapema mwezi huu Ross aliomba radhi ya juu juu kutokana na mashairi yake kwa kutweet: “I dont condone rape. Apologies for the #lyric interpreted as rape. #BOSS”

Baada ya masaa mawili alijaribu kuomba msamaha tena: “Apologies to my many business partners, who would never promote violence against women. @ReebokClassics @ultraviolet”

AIBU: MKE WA MTU ANASWA LIVE AKIFANYA MAPENZI NDANI YA GARI MAENEO YA MWENGE-DAR




KUFUATIA vitendo vya usaliti wa ndoa, uasherati, ufuska na ukiukwaji wa maadili ya Kitanzania kwa wanandoa, wiki iliyopita Ijumaa iliendelea na Operesheni Fichua Maovu kwa kuzunguka jijini Dar usiku wa manane na kunasa tukio la mke wa mtu akifanya uzinzi ndani ya gari.


Kabla ya kufanya operesheni hiyo, waandishi  walitaarifiwa kwamba Wilaya ya Kinondoni jijini Dar ndiyo inayoongoza kwa wake na waume  za watu kufanya vitendo vya ngono kwenye magari.




Maeneo yaliyodaiwa kwamba wazinzi hao hupenda kuyatumia ni Coco Beach, Leaders Club, Mlimani City na sehemu kubwa ya vitongoji vya Sinza na Mwenge, Dar.

Mbali na waume na wake za watu, wengine wanaotajwa kufanya vitendo vya ngono ndani ya magari ni mastaa wakubwa ambao wanaogopa kwenda kukodi vyumba mahotelini na gesti wakihofia watajulikana kutokana na umaarufu wao.
 Jumatatu ya Aprili Mosi, mwaka huu, waandishi wetu walianza mchakato wa kutembelea vitongoji walivyoezwa kwamba, watu hususan wake na waume za watu hupenda kuvitumia kufanyia ufuska.

Waandishi wetu walitinga kwenye Ufukwe wa Coco uliopo Oysterbay, Dar ambako walishuhudia wasichana wengi waliokuwa wakifanya biashara ya kujiuza ‘machangudoa’ katika viunga hivyo.



Mbali na wasichana hao, pia kulikuwa na vibaka wengi waliokuwa wakiwalinda machangudoa hao ili wasipate matatizo.

Pia, wanaume wengi walikuwa wakifika na wanawake ndani ya magari yao na kupozi kwenye maegesho, wengi wao hawakuonekana kama ni watu na wake zao.

 Hata hivyo, waandishi walibaini kwamba magari mengi yanayotumiwa katika eneo hilo ni yale yenye vyoo vyeusi ‘tinted’ hivyo ni vigumu kujua kinachoendelea ndani yake.

Kwa ujanja, waandishi wetu walibaini kwamba ‘pea’ nyingine zilikuwa zikifanya vitendo vya ‘kudendeka’ na wengine kufika mbali zaidi lakini walishindwa kuwavaa kutokana na usalama mdogo katika eneo hilo.


Waandishi  wetu walihamishia mtego wake Leaders Club, Kinondoni mida ya saa 8:05, baada ya kupiga misele ya hapa na waandishi walifanikiwa kumbamba mmoja wa wazinzi.

Waandishi walitulia baada ya kuliona gari aina ya Toyota Land Cruiser  likiwa katika eneo la maficho nje ya viwanja hivyo.

Gari hilo lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba mchezo ulikuwa ukiendelea ndani yake.

Wakati waandishi wakijipanga kulivamia, ghafla waliokuwa ndani walishtuka na kupozi kwa muda.

Hata walipoachiwa ili waendelee, machale yaliwacheza na kuwasha gari kisha kuondoka kwa kasi.


Pamoja na kulikosakosa tukio hilo, waandishi hawakukata tamaa, kuanzia Jumatatu hadi Jumapili waliendelea na utaratibu wa kutembelea viwanja husika.

Jumapili iliyopita baada ya kutembelea viwanja vyote kusaka ‘wahalifu hao’, hatimaye mtego ulinasa.


‘Patroo’ ikiwa kazini maeneo ya Mwenge, Dar jirani kabisa na hoteli moja inayopata umaarufu mkubwa siku za hivi karibu, ghafla gari aina ya Toyota Corona likiwa limepaki kwenye eneo la giza, chini ya mti lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba kulikuwa na watu waliokuwa wakifanya ngono.

Safari hii, bila kufanya makosa, waandishi wetu waliwasogelea ambapo na wao hawakuonekana kujali wapita njia....

UNYAMA: BINTI ANYONGWA KWA KUTUMIA SURUALI YAKE


Tukio hili la kikatili limetokea huko Brazil (Cuiaba public square). Inasemekana kuwa binti huyo mwenye miaka 22 aliuawa na watu kisha wakamning'iniza kwa kutumia suruali yake aina ya jeans ili ionekane kama alijinyonga.

Wazazi wa binti huyo wanamshuku 'x-boyfriend' wake kuwa muhusika wa tukio hilo kwani hawakua na maelewano baina yao siku kadhaa kabla ya tukio.

KAMPUNI YA NDEGE YA FLIGHTLINK YAFANYA KWELI MAONYESHO YA UTALII YA COTMM 2013 JIJINI BEIJING‏

mu2
Mkurugenzi wa Kampuni ya ndege ya Flightlink Capt. Munawer Dhirani akiwa katika picha ya pamoja na na mmoja wa washiriki wa maonyesho hayo kutoka nchini humo.
mu3
Mkurugenzi wa Kampuni ya ndege ya Flightlink Capt. Munawer Dhirani akizungumza na wageni mbalimbali waliomtembelea meza yake kwenye banda la Tanzania katika…
mu2
Mkurugenzi wa Kampuni ya ndege ya Flightlink Capt. Munawer Dhirani akiwa katika picha ya pamoja na na mmoja wa washiriki wa maonyesho hayo kutoka nchini humo.
mu3
Mkurugenzi wa Kampuni ya ndege ya Flightlink Capt. Munawer Dhirani akizungumza na wageni mbalimbali waliomtembelea meza yake kwenye banda la Tanzania katika maonyesho ya utalii ya COTMM 2013 jijini yanayofanyika jijini Beijing China.
mu5
Mkurugenzi wa Kampuni ya ndege ya Flightlink Capt. Munawer Dhirani akimkabidhi jarida maalum la kampuni yake ya Flightlink ofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini China wakati alipotembelea katika banda la Tanzania.