Wanenguaji wa kiume wa Extra Bongo wakionesha mautundu yao.
Wanenguaji wa kike wa Bendi ya Extra Bongo wakifanya yao jukwaani kusindikiza uzinduzi huo.
Msanii mahiri wa ngoma za asili na sanaa za maonesho, One Star akionesha utundu wa kucheza na nyoka stejini.
Majaji wa shindano hilo, John Kitime, Maimatha Jesse na Mussa Husein wakifuatilia shoo ya baadhi ya washiriki (hawapo pichani).
Kigori huyu aligeuka kivutio kikubwa ukumbini humo kwa jinsi ‘alivyochetuka’ na kuonesha manjonjo ya kufa mtu jukwaani.
SHINDANO la kumtafuta Kigori wa Tanzania 2013 limezinduliwa rasmi
jana katika Ukumbi wa SunSiro, Ubungo, jijini Dar ambapo ndani ya ukumbi
huo walipatikana warembo watatu ukumbini humo.Warembo hao wanatarajia kuungana na wenzao ambao wanatarajiwa kufanyiwa usahili hivi karibuni katika mikoa ya Tanga na Morogoro.
0 comments:
Post a Comment