This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, July 6, 2013

PICHA ZA LAANA ZA KUNDI LA BAIKOKO - TANGA

Hizi  ni  baadhi  ya  picha  za  kundi  la  wacheza  uchi / nusu  uchi  maarufu  kwa  jina  la  Baikoko  lenye  maskani  yake Tanga....

 
 
 
 


WAZAZI WAUA MTOTO WAKIGOMBANIA CD YA MSANII "DIAMOND"



Vilio  na  simanzi  vilitanda Jumatano iliyopita Mwananyamala Kisiwani, jijini Dar kufuatia mtoto wa mwaka mmoja, Rahim Rajab kufariki dunia kwa kuangukiwa na watu watatu, akiwemo baba yake mzazi, Rajab Said..


Tukio la watu hao kumwangukia mtoto huyo lilitokea Jumatatu iliyopita na lilisababishwa na ugomvi mkubwa wa CD yenye nyimbo za mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ulioibuka ndani ya chumba cha kulala kati ya mama wa marehemu na mpangaji mwenzake aitwaye Aisha.


Akizungumza kwa machungu kuelezea tukio hilo, mama mzazi wa marehemu Rahim, Habiba Ally alikiri kuwa kisa cha kifo cha mwanaye ni CD tu.Akasema: 

" Kwa kweli hakuna kingine zaidi ya CD, naamini hivyo kwa kuwa mimi sikuwa na ugomvi wowote na Aisha. Tulikuwa tunaishi kawaida tu ukiacha mikwaruzo ya hapa na pale.” 

Akaongeza: Jumamosi iliyopita, Aisha alikuja ndani kwangu na CD zake tatu, ya Diamond, Kingwendu na ya Coast Modern Taarab. Alipomaliza kuangalia aliziacha, akaondoka zake.

“Jumapili mimi nikaenda nazo kwa mama zote tatu kwa ajili ya kuziangalia, tulipomaliza na mimi niliziacha huko. 

“Jumatatu usiku Aisha akaja kunidai, nikamwambia zipo kwa mama. Kwa kuwa anapajua anapoishi mama, si mbali akaenda kuzichukua zote tatu. 


Ajabu aliporudi tu, akaja tena kwangu na kusema hajapewa CD ya Diamond kitu ambacho si kweli na ndipo ulipozuka ugomvi wote huo hadi kusababisha kifo cha mwanangu.”

Akizungumza msibani juzi, bibi wa marehemu, Jamima Hassan alisema siku ya tukio alipigiwa simu na mkwe wake (baba wa marehemu) akamwambia kuna ugomvi nyumbani kwake unaohusu CD kati ya mkewe na mpangaji mwenzake ambapo bibi huyo aliamua kwenda kutatua ugomvi huo.

“Niliondoka muda huohuo kwani huyo Aisha alitoka kwangu kuchukua CD zake muda mfupi tu, sasa nilijiuliza ni CD gani wanazogombania?


“Nilipofika nilikuta ugomvi umepamba moto, baba wa mtoto na mume wa Aisha aitwaye Shaban Sangali walikuwa wameungana kumtoa nje ya chumba Aisha bila mafanikio. 

“Wakati naingia, Aisha alikuwa akitukana matusi mazito na tulipojitahidi kumtoa nje alitusukuma kwa nguvu. Ndipo yeye, mume wake na baba wa mtoto waliwaangukia watoto waliokuwa wamelala kitandani,” alisema bibi huyo.


Akaendelea: Tulipowaangalia watoto ambao ni mapacha, hali zao zilikuwa mbaya, tukaamua kwenda kwa mjumbe wa mtaa kuripoti, akatupa barua, tukaenda Kituo cha Polisi Mwinyijuma, pale wakatupa PF3 ya kuwapeleka Hospitali ya Mwananyamala ambako walilazwa kwa matibabu.


Bibi huyo alisema siku iliyofuata, Rahim alifariki dunia, ikabidi waende Polisi Oysterbay ambapo walifungua shitaka lenye faili kwa kumbukumbu No. OB/RB/1150/2013 MAUAJI.

Watuhumiwa katika RB hiyo ni Aisha na mumewe, Sangali ambao walikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.


Majirani waliozungumza na mwandishi wetu  walisema wakati ugomvi kati ya Aisha na Habiba unatookea, mume wa Habiba alikuwa anarudi kutoka kazini, akakutana na kimbembe hicho.

Walisema aliingilia kati kuamua bila mafanikio. Wakati huo mume wa Aisha alikuwa chumbani kwake na amefungulia muziki wa redio kwa sauti ya juu hivyo hakujua nini kinaendelea kwenye chumba cha mpangaji mwenzake.


Ikaelezwa kuwa, kuna watu walikwenda kumgongea na kumwambia mkewe anapigwa na mume wa Habiba kwa kushirikiana na mkewe.


Ilibidi mwanaume huyo atoke mbio hadi chumbani kwenye ugomvi ambako alikuta baba wa marehemu akijitahidi kuwaamulia wawili hao bila mafanikio.

Habari zinasema mwanaume huyo aliingilia kati kuongeza nguvu lakini katika hali ya kuwalemea, Aisha aliwasukuma wote na kisha wao kuwaangukia watoto hao mapacha waliokuwa wamelala kwenye kitanda kimoja.


Katika hali ya kusikitisha, marehemu amemuacha pacha mwenzake aitwaye Rahima Rajab ambaye ni kulwa.


Wengi wanaamini kuwa maisha ya Rahima yangekuwa ya furaha zaidi kama Rahimu angekuwepo na kwamba itamsononesha sana akikua na kusikia mwenzake alifariki dunia kwa ugomvi wa mama yake na mpangaji mwenzao kisa ni CD ya nyimbo za mwanamuziki.

GPL

LOWASSA AVIONYA VYOMBO VYA DOLA...!


WAZIRI Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amevitaka vyombo vya dola na wafanyabiashara wakubwa nchini, kujenga mahusiano bora kati yao na wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) ili kuondoa tabaka la matajiri na masikini linaloweza kuathiri uchumi wa taifa.

Lowassa aliyasema hayo jana wakati akizungumza na machinga wa eneo la Makoroboi jijini Mwanza, ambao pamoja na mambo mengine aliwachangia sh milioni 20 kwa ajili ya kutunisha mfuko wao.

Mwanasiasa huyo ambaye pia ni mbunge wa Monduli, aliinyoshea kidole Serikali ya chama chake cha Mapinduzi (CCM) na kuitaka ihakikishe inatekeleza kwa vitendo ilani yake inayosisitiza wananchi kuwezeshwa kiuchumi ili kuondoa matabaka.

Huku akishangiliwa na wafanyabiashara hao, Lowassa ambaye aliongozana na baadhi ya makada wa CCM kutoka ndani na nje ya Mwanza, alisema kila mwananchi wa Tanzania lazima ale, ingawa kwa namna tofauti.

Alisema kuwa ili amani iwepo nchini, lazima Jeshi la Polisi na wafanyabiashara wakubwa wawathamini wafanyabiashara wadogo.

“Tunataka tuwasaidie hawa vijana wetu, maana ni nguzo kubwa sana katika maendeleo ya taifa. Ilani ya CCM inasema lazima watu wawezeshwe kiuchumi.

“Kwa maana hiyo katika nchi yetu kila mtu lazima ale. Na kula kwenyewe tunatofautiana, huyu anakula mkate na huyu anakula hiki. Na ili amani iwepo lazima RPC au OCD na wafanyabiashara wawathamini machinga,” alisema Lowassa.

Pia alitahadharisha kuwa endapo wafanyabiashara hao wadogo watadharauliwa katika nchi, lazima watakula sahani moja na matajiri.

Alitumia pia fursa hiyo kukanusha tuhuma dhidi yake kwamba amejilimbikizia mali.

“Wapo baadhi ya watu wanasema hela ninazotoa hizi ni zangu. Mimi sina fedha, ninazotoa ninapewa na marafiki zangu. Mimi si tajiri wa fedha, ila ni tajiri wa marafiki na ushawishi ninao,” alitamba.

Katika hatua nyingine, Lowassa alikataa kuulizwa maswali na wamachinga hao akisema ameandaa kamati itakayoratibu harambee ya kuwachangia kwa lengo la kupata sh bilioni moja.

“Kwa maandalizi ya harambee nitakayorudi tena kuifanya, na ili mjue kwamba nipo makini natoa hundi ya sh milioni 10 na milioni 10 nyingine nitaitoa leo hii,” alisema Lowassa ambaye baadaye aliondoka kwa kutembea kwa miguu hadi Mwanza Hotel.

Chanzo - Tanzania Daima

Monday, June 24, 2013

BARNABA APOTEZA FAHAMU WAKATI WA MAZISHI YA MAMA YAKE

Mwanamuziki Elias Barnabas 'Barnaba' akiweka udongo katika kaburi la mama yake mzazi, Mariamu  Arubeth.
Baada ya kuweka udongo Barnaba akaishiwa nguvu.
Barnaba akiwa kapoteza fahamu wakati wa mazishi ya mama yake.
Akipatiwa huduma ya kwanza.
Baada ya kuzinduka.
Akipelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu.
Mwanamuziki Elias Barnabas 'Barnaba' jana alipoteza fahamu wakati wa mazishi ya mpendwa mama yake mzazi, marehemu Mariamu Arubeth katika makaburi ya Mburahati jijini Dar es Salaam. Hali ya Barnaba ilibadilika baada ya kuweka udongo katika kaburi la mama yake ndipo alipopoteza fahamu na kupatiwa huduma ya kwanza kisha kupelekwa hospitali. GPL inampa pole msanii Barnaba na wanafamilia wote kwa msiba huu.
(Picha kwa hisani ya This is Diamond)

SUGU AGOMA KUOMBA RADHI BAADA YA KUDAI KUWA WAZIRI MKUU NI MPUMBAVU


Juzi, mbunge  wa  mbeya  mjini  alitoa  tusi  zito  kwa  waziri  mkuu  wa  Tanzania  na  kudai  kuwa  Tanzania  haijawahi  kuwa  na  waziri  mkuu  mpumbuvu  kama  yeye...

Kupitia  account  yake  ya facebook, Sugu, ambaye  ni  mbunge  wa  mbeya  amezidi  kusisitiza  kuwa  hawezi  kuomba  msamaha wala  kuifuta  kauli  yake....

Hii   ni  post  yake  facebook:

"...naskia kuwa watu wanasema kwamba eti nimefuta kauli yangu kuhusu waziri mkuu na amri yake kwa polisi kupiga wananchi?!...

Sina sababu ya kufuta wala kuomba radhi, na nasimamia kauli yangu to the end...kwanza 'upumbavu' sio tusi,upumbavu kwa kiingereza ni stupidity-which is lack of knowledge and understanding...

So hata uwe na cheo gani kama ukishindwa kuwa na 'understanding' juu ya madhara ya kauli zako kwa taifa then u r 'stupid'...ambapo kwa kiswahili ndio 'mpumbavu'..."

KIJIJI CHA NGONO CHAFICHULIWA HUKO SINZA,MAKAHABA WAAHIDI KUTOACHA KAZI HIYO

 


NI hakika ‘mtaa wa ngono’ umefumuliwa! Sakata hilo lilijiri saa tisa usiku, Ijumaa iliyopita, Barabara ya Shekilango, kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori jijini Dar eneo ambalo makahaba wameligeuza chumbani

Kwa mujibu wa takwimu za kiserikali, eneo hilo
(kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori) limekubuhu kwa wasichana kujiuza nyakati za usiku huku makao yao makuu yakiwa eneo la Afrika Sana hasa pembezoni mwa Corner Bar.
 

Mmoja wa viongozi wa serikali ya mtaa ya eneo hilo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe , alisema:
 

“Tumejitahidi sana kushirikiana na polisi ili kutokomeza ukahaba eneo hilo lakini wapi! Hawa mabinti ni wabishi, mbaya zaidi wamelifanya eneo hili kuwa la ngono.

“Watoto wetu wanapita usiku pale wanawaona wanavyofanya, wanatuharibia kizazi kijacho, kama wao wamejishindwa wasiwaambukize wengine.”
Siku ya tukio, saa tisa usiku,  askari wa ulinzi shirikishi walijipanga kwa ajili ya kuufumua mtaa huo huku wakiwa na tahadhari kufuatia habari za kiintelijensia kudai kuwa, makahaba hao walipanga kuua mtu punde watakapovamiwa.
 

Askari hao wakiwa kwenye doria ya kila usiku, waliwavamia makahaba hao eneo lenye majani madogo katikati ya Afrika Sana na Mapambano upande wa yadi ya Mwanamboka wakiwa na wateja wao wakifanya ngono hadharani.


Katika hali iliyoonesha makahaba wamejiimarisha kwa ulinzi siku hizi, wakati wa zoezi hilo, machangu hao sanjari na vibaka  wanaowaunga mkono wakisemekana ni ‘walinzi’ wao, waliokota mawe na kuwarushia askari hao hali iliyozua tafrani zaidi.


Ndipo piga nikupige ilipozuka ambapo askari walionesha umahiri wao wa kupambana na wahalifu kwa kuwadhibiti kwa vichapo vya hapa na pale na kufanikiwa kuwaweka wengi chini ya ulinzi.


Kuona hivyo, baadhi ya makahaba na wateja wao walifanikiwa kuwachoropoka askari bila nguo na kutokomea gizani hivyo kulifanya eneo hilo kuwa jeupe.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, baadhi ya makahaba waliokimbia walijikuta wakiacha kwenye majani nguo zao za ndani na kuzua maswali kwamba ni kwa nini hawakuwa wamezivaa!


“Jamani hizi si nguo zao za ndani? Ina maana wakiwa kazini hawavai siyo? Wanakuwa tayaritayari kwa kazi? Jamani!” alisema kwa mshangao mkubwa mmoja wa askari hao.
 
Licha ya kuwa chini ya ulinzi mkali, baadhi ya makahaba walionaswa walikuwa wakiwalalamikia askari hao kwamba wanawafuatafuata wakati kila mtu siku hizi anaangalia atakulaje!
 

“Mnatuonea bure, nyie mnakula kivyenu na sisi mngetuacha tule kivyetu, hao watoto wenu mnaosema tunawaharibu usiku huu wao wanatokea wapi na wanakwenda wapi?” alisikika akisema kahaba mmoja aliyekuwa mtata kuwekwa chini ya ulinzi.


Mwingine akadakia: "Kama mnataka tuwape uroda si mseme, mnatukamata kila siku kwani tunawatibulia nini majumbani mwenu? Lini tumekuja kuwaghasi wakati mmelala na wake zenu?”
 

Uchunguzi wa kawaida ulibaini kuwa muda rasmi wa 
makahaba hao kuwasili eneo la Corner Bar ili kuanza ‘kazi’ ni saa mbili usiku japokuwa wapo wanaoripoti mapema na kufanya biashara hiyo kwa wizi kulingana na wateja wenye ‘kiu’ nyakati hizo.

Licha ya kuwa chini ya ulinzi, makahaba hao waliahidi endapo watapelekwa polisi na kutoka watarejea eneo hilo kujiuza kwani ndiyo ajira inayowafanya waendelee kuishi katika Jiji la Dar es Salaam, kusomesha watoto vijijini kwao na kuwasaidia wazazi wao mahitaji mbalimbali.
 

“Hata kama mtatupeleka polisi, tutarudi tu hapa, sisi tunasomesha watoto, tunasaidia wazazi wetu vijijini, pia tunaishi Dar kwa sababu ya kipato hiki cha kuuza miili yetu, acheni hizo,” mmoja wa makahaba hao alisema bila kumung’unya maneno.

WABUNGE NA MASHOGA WATETA.....HOFU YA KUWA NA RAIS SHOGA TANZANIA YATANDA


WABUNGE wanachama wa Chama cha Kupambana na Ukimwi (TAPAC), wiki iliyopita walikutana na kujadiliana mambo mbalimbali na mashoga katika mkutano wa mwaka wa chama hicho uliofanyika kwa muda wa siku tatu mjini  Dodoma. Katika mkutano huo, baadhi ya wabunge walionyesha wasiwasi wa taifa kupata rais shoga katika miaka ijayo kutokana na ongezeko la mashoga hapa nchini.

Mbali na wasiwasi ulioonyeshwa na wabunge, mashoga waliokuwa wakihudhuria mkutano huo, walilalamikia vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa na wanajamii wenzao na kudai watambulike na wapatiwe huduma za msingi za kibinadamu.

Akizungumza katika mkutano huo uliomalizika jana, Mbunge wa Nkasi, Ally Kessy (CCM), alitahadharisha uwezekano wa nchi kupata rais shoga katika miaka ijayo, iwapo hatua za makusudi za kudhibiti hali hiyo hazitachukuliwa.

“Tabia ya kuwapeleka watoto kwenye shule za mabweni wangali wadogo wa umri wa miaka hadi miwili, itatuletea matatizo baadaye.

“Katika shule nyingi za bweni vitendo vichafu vinafanyika, vikiwamo vya ushoga. Katika vyuo vikuu hivi sasa kuna mashoga wasiopungua 40,000. Hii ni hatari, tusipojihadhari tutakuwa na rais shoga katika miaka ijayo,” alisema Kessy huku akishangiliwa na wabunge.

Mbunge huyo alitaka elimu dhidi ya ushoga na athari zake ienezwe nchini kupitia vyombo vya habari na nyumba za ibada.

Naye, mmoja wa mashoga waliohudhuria mkutano huo aliyejitambulisha kwa jina la Abdilah Ally, alieleza kuwa yeye ni shoga mwenye wanaume watatu lakini amekuwa akikutana na vitendo vya unyanyasaji kutoka ndani ya jamii inayomzunguka.

“Tunataka haki zetu. Tunanyanyaswa katika jamii hasa na polisi. Na sisi tunastahili huduma bora za afya na nyingine tuweze kujikinga na Ukimwi,”
alisema Ally, mkazi wa Dar es Salaam.

Wakati huo huo, taarifa iliyotolewa na Mshauri wa Masuala ya Ufundi wa Kampuni ya Jhpiego, Dk. Augustine Hellar, ilieleza kuwa kuna wanaume 397,458 waliotahiriwa nchini hadi Mei, mwaka huu katika mpango maalumu wa tohara kwa ajili ya kupambana na maradhi ya Ukimwi.

Dk. Hellar alitoa takwimu hizo alipowasilisha mada kuhusu tohara ya hiari kwa wanaume katika kukabili maambukizi ya Ukimwi nchini.

Alisema lengo la mpango huo ulioanza kutekelezwa Oktoba, 2011 katika baadhi ya mikoa nchini ni kutoa tohara kwa wanaume milioni 2.8 kila mwaka mmoja.

Alisema mpango huo umekabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwamo ya watu wazima ambao ndiyo walengwa kutojitokeza kwa wingi na baadhi ya watu kuhusisha hatua hiyo na upotevu wa nguvu za kiume.