Tanzania
bado ipo kwenye mgogoro na nchi ya Malawi juu ya mpaka halisi wa
nchi,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Benard Membe
amesema hatma juu ya mgogoro huo inategemewa kutolewa mwezi march.
Hukumu hiyo itaamuliwa baada ya jopo la Usuluhishi litakapokaa na
kusikiliza pande zote mbili ambalo litaongozwa na Rais wa zamani wa
Msumbiji Joachim Chisano
Kupatikana kwa suluhu ya mgogoro wa mpaka huo kutawatoa hofu wananchi
wanaoishi pembezoni mwa Ziwa hilo ambao wamekuwa wakitegemea shughuli
za uvuvi wakiwemo wakazi wa kijiji cha Manda Jimbo la Ludewa mkoani
Njombe.
Wakazi wa eneo hilo wamesema kwa hivi karibuni tangu kutulia kwa
vuguvugu la mgogoro huo wamekuwa wakiendelea shughuli zao za maendeleo
kama kawaida ikiwemo uvuvi.
Friday, February 21, 2014
Home »
» Kilichosemwa na Mh.Membe kuhusu Mgogoro wa Mpaka kati ya Tanzania na Malawi.
0 comments:
Post a Comment